Michuano ya ligi ya Muungano 2026 inatarajiwa kuanza visiwani Zanzibar April 21 ikitarajiwa kushirikisha timu nane ambapo nne zitatoka Zanzibar na nne zikitoka Tanzania Bara.
Timu za Yanga, Simba, Azam Fc na Singida Black Stars zinatarajiwa kushiriki zikitokea Tanzania Bara huku Mlandege FC, Muembe Makumbi City, Mafunzo na KVZ zikitokea Zanzibar.





