Klabu ya Yanga imethibitisha kupokea taarifa rasmi kutoka kwa Bodi ya ligi kuwa mchezo wake dhidi ya Tanzania Prisons utapigwa Alhamisi, March 12 katika uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma.
Kumekuwa na mkanganyika juu ya wapi mchezo huo utapigwa jana Tanzania Prisons ikitangaza kuchagua uwanja wa Ali Hassan Mwinyi huku kikosi cha timu hiyo kikiwasili Tabora mapema leo.





