Local,Normal News,Simba, Singida, TRA, Dodoma, Azam, Namungo

Mechi za ligi kuu leo Jumatano, March 11

Joel JJ By Joel JJ
β€’
11 Mar 2026
Mechi za ligi kuu leo Jumatano, March 11

Mikiki mikiki ya ligi kuuya NBC inaendelea leo kwa mechi za viporo kupigwa katika viwanja mbalimbali.

Timu ya TRA United itakuwa mwenyeji wa Namungo Fc katika mchezo wa mapema utakaopigwa saa nane mchana katika uwanja wa Black Rhino Arusha.

Majira ya saa 10:15 jioni mchezo unaosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka nchini kati Singida BS dhidi ya Simba utapigwa uwanja wa Airtel Mtipa huku Singida.

Hii ni mechi inayowakutanisha miamba wawili ambao wote walikuwa na majukumu ya michuano ya Kimataifa msimu huu Simba ikicheza ligi ya mabingwa na Singida BS kombe la Shirikisho.

Timu hizo zimekuwa na ushindani wa aina yake kila zinapokutana ambapo mara ya mwisho Singida BS waliibuka na ushindi wa mabao 3-1 katika mchezo wa nusu fainali kombe la CRDB msimu uliopita.

Saa 1:15 usiku, Dodoma Jiji watahitimisha mechi za leo kwa mchezo dhidi ya Azam Fc uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma.

Azam Fc wamekosa ushindi katika mechi mbili zilizopita pengine leo watashuka uwanjani wakiwa na dhamira ya kuondoka na alama zote tatu.

Hata hivyo wanakutana na Dodoma Jiji ambayo msimu huu imejipambanua kwa kutopoteza mchezo kwenye uwanja wake wa nyumbani.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’