Local,Normal News,Azam, Dodoma

Dodoma Jiji hoi mbele ya Azam Fc, yapigwa 3-0

Joel JJ By Joel JJ
β€’
11 Mar 2026
Dodoma Jiji hoi mbele ya Azam Fc, yapigwa 3-0

Dodoma Jiji 'wametepeta' uwanja wa nyumbani, Jamhuri mkoani Dodoma wakikubali kipigo cha mabaoo 3-0 kutoka kwa Azam FC katika mchezo wa ligi kuu ya NBC.

Zidane Seleli alikuwa shujaa wa Azam Fc katika mchezo huo akifunga mabao mawili dhidi ya waajiri wake wa zamani huku Feisal Salum 'Fei Toto' akirejea na bao na asisti baada ya kumaliza adhabu ya kukosa mechi mbili kufuatia kadi nyekundu aliyopata katika mchezo dhidi ya Pamba Jiji.

Baada ya kukosa ushindi katika mechi mbili zilizopita, hatimaye Azam Fc imerejea katika mwendo wa kukusanya alama tatu, ushindi huo ukiwasogeza hadi nafasi ya tatu kwenye msimamo kwa tofauti ya mabao baada ya kufikisha alama 27 sawa na Simba liyopata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Singida BS katika mchezo wa mapema.

Mchezo unaofuata kwa Azam Fc ni dhidi ya Yanga, utakaopigwa March 15 katika uwanja wa Benjamini Mkapa, dabi ya Dar es salaam.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
3h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
3h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
4h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
4h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
5h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
6h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
6h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
20h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
21h ago
READ MORE β†’