TRA United yaipeleka Simba Sheikh Amri Abeid, Arusha

Joel JJ By Joel JJ β€’ 12th March 2026


TRA United yaipeleka Simba Sheikh Amri Abeid, Arusha

Mchezo wa Ligi Kuu ya NBC kati ya TRA United na Simba SC utapigwa kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha.

Afisa habari TRA United, Christina Mwagala amethibitisha hilo wakati akitoa taarifa kwa vyombo vya habari.

TRA iliuchagua uwanja wa Black Rhino, Karatu kama uwanja wao wa nyumbani na jana ilicheza dhidi ya Namungo na kupata ushindi wa mabao 2-0.

Kutokana na ukubwa wa mchezo huo klabu imetangaza kutumia uwanja wa Sheikh Amri Abeid badala ya Black Rhino.

Mchezo huo utapigwa saa 10:00 Jioni, Jumamosi March 14 2026.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.