Mchezo wa Ligi Kuu ya NBC kati ya TRA United na Simba SC utapigwa kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha.
Afisa habari TRA United, Christina Mwagala amethibitisha hilo wakati akitoa taarifa kwa vyombo vya habari.
TRA iliuchagua uwanja wa Black Rhino, Karatu kama uwanja wao wa nyumbani na jana ilicheza dhidi ya Namungo na kupata ushindi wa mabao 2-0.





