Mkataba wambana beki TRA United kucheza dhidi ya Simba

Joel JJ By Joel JJ β€’ 13th March 2026


Mkataba wambana beki TRA United kucheza dhidi ya Simba

Timu ya TRA United iliyohamishia makazi yake mkoani Arusha, kesho Jumamosi March 14 itakuwa mwenyeji wa Simba katika mchezo wa ligi kuu ya NBC.

Katika mchezo huo TRA United watamkosa beki wao tegemeo Chamou Karabou ambaye anatumikia timu hiyo kwa mkopo akitokea klabu ya Simba.

Makubaliano ya kimkataba baina ya TRA United na Simba, yanamzuia Chamou kucheza dhidi ya waajiri wake hao, klabu ya Simba.

Chamou amekuwa na kiwango kizuri tangu ajiunge na TRA United akiwa ameifungia timu hiyo moja ya mabao kwenye ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Namungo Fc katika mchezo uliopita.

Hata hivyo TRA United wanaweza kumtumia kiungo 'punda' Mzamiru Yassin ambaye nae alijiunga na timu hiyo kwa mkopo kwenye usajili wa dirisha dogo akitokea klabu ya Simba.

Valentine Nouma ni mchezaji mwingine ambaye pia anaitumikia TRA United akiwa nae amewahi kupita kunako klabu ya Simba.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.