Mchezo wa ligi kuu ya NBC kati ya TRA United dhidi ya Simba uliokuwa upigwe leo Jumamosi March 14 saa 10 jioni katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha, haujafanyika kutokana na mvua kubwa iliyonyesha na kupelekea uwanja kujaa maji.
Kamishna wa mchezo huo, Mussa Nyamandege ameuahirisha kwa kuzingatia matakwa ya kikanuni.
Taarifa zaidi kuhusu hatma ya mchezo inatarajiwa kutolewa na badae na Bodi ya ligi



