Berkane chupuchupu nyumbani mbele ya Al Hilal katika Robo Fainali CAF Champions League

Joel JJ By Joel JJ β€’ 15th March 2026


Berkane chupuchupu nyumbani mbele ya Al Hilal katika Robo Fainali CAF Champions League

Klabu ya RS Berkane ya Morocco imelazimishwa sare ya 1–1 na Al Hilal Omdurman ya Sudan katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa robo fainali ya mashindano ya CAF Champions League uliochezwa Jumamosi, Machi 14, 2026 kwenye Uwanja wa Municipal mjini Berkane.

Mchezo huo ulikuwa wa ushindani mkubwa huku kila timu ikijaribu kupata faida kabla ya mchezo wa marudiano utakaopigwa Sudan.

Wageni Al Hilal ndio waliokuwa wa kwanza kupata bao la kuongoza mapema katika mchezo huo baada ya mshambuliaji Abu Aqla Omer kufunga dakika ya 13, akimalizia vizuri pasi ya Abdelraouf Yagoub na kuwapa timu yake matumaini ya ushindi ugenini.

Baada ya bao hilo, Berkane waliongeza kasi ya mashambulizi wakitafuta kusawazisha lakini walikutana na upinzani mkali kutoka kwa safu ya ulinzi ya Al Hilal ambayo ilisimama imara kwa muda mrefu wa mchezo.

Hata hivyo, juhudi za wenyeji zililipa katika dakika za mwisho za mchezo baada ya Berkane kupata penati katika dakika za nyongeza, ambapo mshambuliaji Youssef Mehri alifunga bao la kusawazisha na kufanya matokeo kuwa 1–1.

Bao hilo la dakika za mwisho limeifanya mechi ya marudiano kuwa wazi kwa timu zote mbili zitakapokutana tena Rwanda wiki ijayo kuwania tiketi ya kufuzu hatua ya nusu fainali

Kwa mujibu wa ratiba ya mashindano ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF), mshindi wa jumla kati ya RS Berkane na Al Hilal atakutana na mshindi wa mchezo kati ya AS FAR Rabat na Pyramids FC katika hatua ya nusu fainali.Β 

Hatua ya robo fainali ya CAF Champions League inaendelea leo kwa mchezo mwingine mkubwa utakaowakutanisha Esperance Sportive de Tunis ya Tunisia dhidi ya mabingwa wa kihistoria wa mashindano hayo, Al Ahly ya Misri.Β 


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.