Klabu ya Real Madrid imepata ushindi muhimu wa mabao 4–1 dhidi ya Elche CF katika mchezo wa La Liga uliochezwa Jumamosi, Ma"> Klabu ya Real Madrid imepata ushindi muhimu wa mabao 4–1 dhidi ya Elche CF katika mchezo wa La Liga uliochezwa Jumamosi, Ma">

Real Madrid wapunguza pengo kwa Barcelona baada ya ushindi mkubwa La Liga

Joel JJ By Joel JJ • 15th March 2026


Real Madrid wapunguza pengo kwa Barcelona baada ya ushindi mkubwa La Liga

Klabu ya Real Madrid imepata ushindi muhimu wa mabao 4–1 dhidi ya Elche CF katika mchezo wa La Liga uliochezwa Jumamosi, Machi 14, 2026 kwenye Uwanja wa Santiago Bernabeu Stadium. Ushindi huo umeifanya Real Madrid kuendelea kuweka presha katika mbio za ubingwa wa ligi ya Hispania wakiwa nyuma ya vinara Barcelona kwa tofauti ya alama moja. .

Real Madrid walipata bao la kwanza dakika ya 38 kupitia beki Antonio Rüdiger, aliyefunga baada ya mpira wa adhabu uliopigwa na Federico Valverde kugonga ukuta na kumrudia ndani ya eneo la hatari. Dakika ya 44, kiungo Federico Valverde aliongeza bao la pili kwa shuti kali kutoka nje ya eneo la hatari na kuifanya Madrid kuongoza mabao 2–0 kabla ya mapumziko.

Kipindi cha pili kilianza kwa presha zaidi kutoka kwa wenyeji na katika dakika ya 65, beki kijana Dean Huijsen aliifungia Real Madrid bao la tatu kwa kichwa kufuatia krosi iliyopigwa kutoka upande wa kulia.

Elche CF walipata bao lao pekee dakika ya 84 baada ya kiungo wa Real Madrid Manuel Ángel kujifunga wakati akijaribu kuokoa mpira uliokuwa unaelekea golini. Hata hivyo, Real Madrid walihitimisha ushindi wao kwa bao la nne lililofungwa na kiungo Arda Güler dakika ya 88, aliyefunga bao la kuvutia kwa shuti refu lililomshinda kipa aliyekuwa ametoka nje ya lango.

Katika mchezo mwingine wa siku hiyo, Atlético Madrid waliibuka na ushindi mwembamba wa 1–0 dhidi ya Getafe CF katika mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa Metropolitano Stadium.

Bao pekee la mchezo huo lilifungwa na beki wa Atletico Nahuel Molina katika kipindi cha kwanza na kuwapa wenyeji pointi tatu muhimu katika mbio za kusalia katika nafasi za juu za ligi. 

Mchezo huo pia ulitawaliwa na tukio la utata baada ya beki wa Getafe Abdel Abqar kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 55 kufuatia tukio lililogunduliwa kupitia VAR la kumshika vibaya mshambuliaji Alexander Sørloth, huku Sørloth akionyeshwa kadi ya njano kwa kulipiza kisasi. 

Kwa matokeo hayo, Real Madrid wanaendelea kusalia kwenye ushindani wa juu katika mbio za ubingwa wa La Liga, huku Atlético Madrid wakishikilia nafasi ya tatu.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.