Local,Normal News,Yanga, Azam

Ni Azam Fc vs Yanga leo, Dar Derby

Joel JJ By Joel JJ
β€’
15 Mar 2026
Ni Azam Fc vs Yanga leo, Dar Derby

Mikiki mikiki ya ligi kuu ya NBC inaendelea leo ambapo michezo miwili inatarajiwa kupigwa katika viwanja tofauti.

Mchezo wa mapema saa 10, Mbeya City itaikaribisha Singida BS katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Babati mkoani Manyara.

Mchezo huo utafuatiwa na mechi kubwa inayosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka nchini, dabi ya Dar es salaam kati ya Azam Fc dhidi ya Yanga utakaopigwa saa 2:30 usiku katika uwanja wa Benjamin Mkapa.

Unapozungumzia dabi, Azam Fc na Yanga pengine ndio dabi yenye ushindani zaidi pengine kuliko hata ile ya Kariakoo kwa kuangalia matokeo ya mechi za karibuni.

Msimu uliopita Azam Fc walishinda mchezo mmoja na Yanga pia wakashinda mchezo mmoja huku kila timu ikifunga mabao mawili katika mechi hizo mbili.

Msimu huu ni Azam Fc na Yanga pekee ambazo hazijapoteza mchezo kwenye ligi mpaka sasa.

Yanga ndio vinara wa ligi wakikusanya alama 35 baada ya mechi 13 wakati Azam Fc wakishika nafasi ya tatu wakikusanya alama 27 baada ya mechi 13 pia.

Mara ya mwisho timu hizo zilikutana kwenye fainali ya michuano ya kombe la Mapinduzi mwezi Januari mwaka huu Yanga ikiibuka mabingwa kwa mikwaju ya penati baada ya matokeo ya suluhu ya bila kufungana.

Ni wazi zitakuwa dakika 90 ngumu kwa kila upande lakini zenye burudani ya aina yake kwa mashabiki wa soka nchini.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’