Local,Normal News,Azam, Yanga

Azam Fc, Yanga hakuna mbabe

Joel JJ By Joel JJ
β€’
16 Mar 2026
Azam Fc, Yanga hakuna mbabe

Mchezo wa ligi kuu ya NBC kati ya Azam Fc dhidi ya Yanga uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa, umemalizika kwa matokeo ya suluhu ya bila kufungana.

Ni mchezo uliotawaliwa na ufundi mwingi lakini nafasi chache zikitengenezwa na kila upande pengine kutokana umakini uliokuwa eneo la ulinzi kwa timu zote.

Azam Fc ilianza mchezo huo kwa kasi na mapema tu walimpa kazi mlinda lango wa Yanga Djigui Diarra kuokoa hatari langoni.

Hata hivyo kipindi cha pili ni Yanga iliyokuwa bora zaidi ikitawala mchezo kwa muda mwingi lakini uimara wa Azam Fc kuanzia eneo la kiungo liliwapa wakati mgumu washambuliaji wa Yanga kupenya.

Dakika za lala salama mshambuliaji Prince Dube aliangushwa ndani ya eneo la hatari lakini mwamuzi wa mchezo huo 'akapotezea' tukio hilo ambalo pengine lingeipa Yanga nafasi ya kufunga.

Ni alama moja kwa kila timu Yanga ikiendelea kusalia kileleni na alama 36 huku Azam Fc wakisogea nafasi ya pili wakifikisha alama 28.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
45m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’