Laporta ashinda uraisi wa Barcelona kwa mara ya nne

Joel JJ By Joel JJ • 16th March 2026


Laporta ashinda uraisi wa Barcelona kwa mara ya nne

Katika uchaguzi wa uongozi wa klabu ya FC Barcelona uliofanyika Jumapili, Machi 15, 2026, Joan Laporta ameshinda tena nafasi ya urais wa klabu hiyo kwa kishindo na kupewa dhamana ya kuiongoza Barcelona kwa muda wa miaka mitano ijayo.

Matokeo rasmi ya uchaguzi yameonyesha kuwa Laporta alipata zaidi ya 68% ya kura, akishinda dhidi ya mpinzani wake mkuu Víctor Font ambaye alipata karibu 30% tu ya kura zilizopigwa.

Hii ni mara ya nne kwa Laporta kushika nafasi ya rais wa Barcelona, na ya pili mfululizo tangu alipochaguliwa tena mwaka 2021. Ushindi huu unamaanisha kuwa atabakia kiongozi wa klabu hiyo hadi mwaka 2031, akiwa na jukumu la kuendelea na miradi mikubwa ya klabu, pamoja na uimarishaji wa kikosi cha soka, kukamilisha ujenzi wa ubunifu wa uwanja wa Camp Nou, na kulinda maslahi ya klabu kimataifa.

Katika hotuba yake ya ushindi, Laporta alishukuru sana wanachama wa klabu kwa kuonyesha imani naye na kuahidi kuwafanyia kazi kwa bidii kwa maslahi ya Barcelona. Alisema matokeo hayo yanampa nguvu ya kusonga mbele na miradi ya maendeleo kabisa, akiwa amejizolea uimara mkubwa kutoka kwa wanachama waliojitokeza kupiga kura.

Uchaguzi huo ulihudhuriwa na wanachama wengi wa Barcelona, na ushindi wa Laporta unaonekana kuleta hali ya matumaini kwa mashabiki, wengi wakiona kuwa utatoa utulivu wa uongozi na kuendeleza mafanikio ya kikosi cha soka chini ya kocha Hansi Flick. Athari za maamuzi yake ya uongozi, miongoni mwa nyingine kukamilisha mradi wa upanuzi wa Camp Nou na mikakati ya kifedha, zilizungumziwa sana wakati wa kampeni za uchaguzi.

Kwa ujumla, ushindi huu wa Laporta ukochochea mjadala mpana kati ya wapenda soka, huku wengi wakitarajia kuona Barcelona ikipata mafanikio makubwa zaidi, ndani na nje ya uwanja, wakati wa muhula huu mpya wa uongozi. Hansen Flick na wachezaji kama Lamine Yamal pia wamepata sapoti kubwa kutoka kwa wanachama, na wengi wanatarajia kuwa muunganiko wa uongozi mzuri utaungwa mkono na mafanikio ya kikosi cha kwanza. 


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.