Soko la usajili barani Ulaya linaendelea kupamba moto huku vilabu vikubwa vikianza kupanga mikakati ya msimu ujao. Tetesi za Jumanne zinaonyesha wazi kuwa vita ya kuwania wachezaji chipukizi na nyota waliothibitisha ubora wao imezidi kushika kasi.
Vita ya Manchester United na Bayern Munich kwa Anderson
Kiungo wa Nottingham Forest, Elliot Anderson, ameibuka kuwa mmoja wa wachezaji wanaowaniwa zaidi kwa sasa. Manchester United wanatajwa kuonyesha nia kubwa ya kumsajili, lakini watakutana na upinzani mkali kutoka Bayern Munich ambao nao wako tayari kuingia vitani kumsaka kiungo huyo mwenye umri wa miaka 23.
Mustakabali wa Morgan Rogers watikisa Aston Villa
Katika Aston Villa, winga Morgan Rogers anaweza kulazimika kutafuta changamoto mpya ikiwa timu hiyo haitafanikiwa kufuzu Ligi ya Mabingwa Ulaya. Mchezaji huyo anatajwa kutaka kucheza katika kiwango cha juu zaidi barani Ulaya.
Mashaka yaendelea Arsenal
Kuna hali ya sintofahamu ndani ya Arsenal kuhusu mustakabali wa baadhi ya nyota wao chipukizi. Gabriel Martinelli anatajwa kuwa na mustakabali usioeleweka, huku majina ya Myles Lewis-Skelly na Ethan Nwaneri nayo yakitajwa katika mjadala wa mwelekeo wa baadaye wa kikosi hicho.
Newcastle United wahofia kumpoteza Sandro Tonali
Newcastle wanakabiliwa na presha kubwa baada ya kiungo wao Sandro Tonali kuhusishwa na uhamisho wa pauni milioni 100. Vilabu vikubwa kama Manchester United, Manchester City, Chelsea na Real Madrid vinatajwa kumuwania nyota huyo wa Italia.
Nathan Aké aibua mvutano Italia
Beki wa Manchester City, Nathan Aké, anahusishwa na kuhamia Italia huku AC Milan na Inter Milan zikitajwa kuonyesha nia ya kumsajili, kufuatia kukosa nafasi ya kudumu katika kikosi cha kwanza cha City.
Riccardo Calafiori abaki Arsenal
Licha ya kuhitajika na vilabu vikubwa vya Italia kama Inter Milan, AC Milan, Juventus na Napoli, Arsenal hawana mpango wa kumuuza beki wao Riccardo Calafiori katika dirisha lijalo.
Liverpool wamnyatia Eduardo Camavinga
Liverpool wanaendelea kusaka kiungo wa ubora wa juu, na sasa wanamuwania nyota wa Real Madrid, Eduardo Camavinga. Uhamisho huu unaweza kuwa moja ya dili kubwa zaidi msimu wa joto.
Jonathan David avutia England
Mshambuliaji wa Canada, Jonathan David, yuko sokoni huku Juventus wakisikiliza ofa. Vilabu vya England kama West Ham United, Tottenham Hotspur na Nottingham Forest vinatajwa kumuhitaji.
Paris Saint-Germain wasimama kidete kwa Khvicha Kvaratskhelia
PSG wameweka wazi kuwa hawana mpango wa kumuachia Khvicha Kvaratskhelia licha ya kuhusishwa na Arsenal. Nyota huyo wa Georgia anaendelea kuwa sehemu muhimu ya kikosi hicho.
Lorenzo Pellegrini kwenye rada ya Juventus
Nahodha wa AS Roma, Lorenzo Pellegrini, anaweza kuondoka klabuni hapo bure mwishoni mwa msimu. Juventus wanatajwa kuwa mstari wa mbele kuwania saini yake.



