Real madrid wako kwenye mazungumzo na beki wao raia wa Ujerumani mwenye umri wa miaka 33, Antony rüdiger, kuhusu kuongeza mkataba mpya.
Mkataba wa Rüdiger unatarajiwa kumalizika majira ya joto, huku taarifa zikieleza kuwa pande zote mbili zinaonyesha nia ya kuendelea na ushirikiano huo. Uongozi wa Madrid unaona umuhimu wa kubaki na beki huyo mwenye uzoefu, hasa katika kipindi hiki ambacho klabu inahitaji uimara zaidi safu ya ulinzi.
Wakati huohuo, Madrid wanahitaji beki mwenye uzoefu kikosini, hasa ikizingatiwa kuwa David alaba anatarajiwa kuondoka klabuni hapo.
(Chanzo: MARCA in English)



