Aishi Manula amepambana na magumu yote, sasa amerejea kwenye ubora

Joel JJ By Joel JJ β€’ 20th March 2026


Aishi Manula amepambana na magumu yote, sasa amerejea kwenye ubora

Katika kipindi ambacho wengi walidhani mlinda lango Aishi Manula ameisha kutokana na umri na jeraha, golikipa huyo wa taifa na wa klabu ya Azam FC amerudi kwa nguvu zake kamili, akithibitisha kuwa hadithi za sifa mbaya zilikuwa mbali na ukweli.

Safari ya Kurudi Uwezo

Baada ya kupata jeraha lililomfanya akae nje ya uwanja kwa muda mrefu na baadae kuachwa na waliokuwa waajiri wake wa zamani klabu ya Simba, Manula alikumbwa na maoni hasi na baadhi ya watu waliodhani alikuwa amemaliza kazi yake ya soka.

Lakini mchezaji huyo, kwa heshima na uvumilivu, alikubali hali hiyo bila kuwakosea heshima wale waliokuwa wakishiriki katika maisha yake ya awali ya soka.

Mazoezi makali na kujituma bila kuchoka ndicho kilichomsaidia kurudisha kiwango chake cha juu. Matokeo yake sasa Manula amerudi kuwa tegemeo katika klabu yake ya Azam FC na pia akirejeshwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars'.

Unaweza kusema Manula ni mfano wa kuigwa kwa magolikipa wengine wazawa ambao wana ndoto ya kufanya mambo makubwa kwenye soka la Tanzania. Kila hatua yake, kila hatua yake inafundisha vijana jinsi ya kujituma na kudumisha kiwango bila kujali changamoto.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.