Yanga yakwama Dodoma, sare ya tatu mfululizo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 21st March 2026


Yanga yakwama Dodoma, sare ya tatu mfululizo

Bao la dakika za lala salama lililofungwa na Mtibwa Sugar kupitia mpira wa kona uliopigwa na Ismail Mhesa limewanyima Yanga alama tatu muhimu katika mchezo wa ligi kuu uliopigwa uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma.

Wachezaji wa Yanga walimlalamikia mwamuzi kwa kuruhusu bao hilo licha ya mlinda lango Djigui Diarra kuonekana amesukumwa wakati akijaribu kuokoa mpira huo wa kona.

Yanga ilikuwa na kwanza kufunga bao la uongozi kupitia kwa Pacome Zouzoua kwenye kipindi cha kwanza akimalizia pasi ya Emmanuel Mwanengo.

Hata hivyo wachezaji wa Yanga watajilaumu wenyewe kwa kushindwa kuondoka na alama tatu katika mchezo huo kwani walitengeneza nafasi nyingi lakini changamoto ilikuwa katika kuweka mpira kimiani.

Ni sare ya tatu mfululizo Yanga inapata, pengine ni nyakati ngumu zaidi kutokea kwa Yanga kwenye ligi katika misimu ya karibuni.

Msimu uliopita Yanga ilipoteza mechi mbili mfululizo lakini wakati huu sare tatu mfululizo, Yanga ikianza kwa kuchechea mechi za duru ya pili.

Licha ya matokeo hayo, Yanga inaendelea kusalia kileleni mwa msimamo wa ligi ikifikisha alama 38, na kimahesabu wataendelea kuwa kileleni hata ikitokea timu nyingine zitashinda mechi zao za viporo.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.