Klabu ya Al Ittihad SC Tripoli ya Libya imeanza rasmi enzi mpya chini ya kocha wake mkuu, Rulani Mokwena, baada ya kuwasili mjini Fes kwa ajili ya kambi ya mazoezi ya siku 10.
Hatua hiyo inakuja ikiwa ni wiki moja tu tangu kocha huyo raia wa Afrika Kusini atangazwe rasmi kuinoa timu hiyo mnamo Machi 17, 2026, akitokea klabu ya MC Alger ya Algeria.





