Shirikisho la soka la Ulaya, UEFA, limethibitisha kwamba timu itakayomaliza nafasi ya 7 katika ligi ya Premier League msimu huu inaweza kupata nafasi ya kushiriki katika michuano ya UEFA Champions League ya msimu wa 2026-27, iwapo;
Kama Aston Villa watashinda taji la UEFA Europa League na kumaliza katika nafasi ya 5 au 6 kwenye ligi ya Premier League, basi nafasi ya 7 itakuwa na uwezekano wa kuingia Champions League.
Pia, ikiwa Liverpool watashinda taji la UEFA Champions League na kumaliza katika nafasi ya 5 au 6 kwenye ligi ya Premier League, basi pia timu ya 7 itakuwa na nafasi ya kushiriki katika michuano hiyo ya mabingwa barani Ulaya.
Uamuzi huu wa UEFA unaweka uwiano wa haki kati ya mashindano ya ndani.