Kiungo mshambuliaji wa Simba Morice Abraham ameongezwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' kinachojiandaa na mashindano ya FIFA Series yatakayofanyika Rwanda katika kipindi hiki cha mapumziko ya kalenda ya FIFA.
Kocha Mkuu wa Stars Miguel Gamondi amethibitisha kuongezwa kwa Abraham ambaye amechukua nafasi ya Simon Msuva aliyeshindwa kujiunga na timu.
"Msuva ameshindwa kuja nchini kutokana na hali ya Iraq, imekuwa ngumu kupata ndege kwa wakati hivyo nafasi yake tumemuita Morice Abraham."
"Tunaendelea vyema na maandalizi yetu ambapo tunatarajiwa leo wachezaji wanne ambao bado hawakuwa wamewasili kambini wataripoti," alisema.
Tanzania itashiriki 2026 FIFA Series Kigali, Rwanda, michuno inayotarajiwa kuanza March 26β30, 2026, uwanja wa Pele. Tanzania imepangwa kundi Group B pamoja na Liechtenstein, Aruba, na Macau
Mechi ya kwanza watacheza March 26, 2026, dhid ya Liechtenstein. Michuano hii iko ndani ya kalenda ya FIFA.