International,Normal News,Coventry city,Frank lampard,Chelsea, EFL, Local

Lampard na Coventry mambo mazuri, Chelsea wampigia chapuo kurudi darajani

Xtra 90 Media By Xtra 90 Media
β€’
24 Mar 2026
Lampard na Coventry mambo mazuri, Chelsea wampigia chapuo kurudi darajani

Kocha wa Coventry City, Frank Lampard, yuko mbioni kuweka historia mpya ndani ya klabu hiyo, huku wito ukizidi kuongezeka kuhusu uwezekano wa kurejea kwake katika katika klabu ya Chelsea.

Lampard alichukua mikoba ya kuinoa Coventry mwaka 2024 wakati timu hiyo ikiwa kwenye hatari ya kushuka daraja, lakini tangu wakati huo ameiongoza katika mabadiliko makubwa na ya kushangaza. Chini ya uongozi wake, Coventry imepanda hadi nafasi za mtoano wa kupanda daraja, kufika kileleni mwa msimamo wa EFL Championship, na kuweka tofauti ya pointi tisa dhidi ya wapinzani wao.

Aidha, timu hiyo imeonyesha makali makubwa katika safu ya ushambuliaji, ikiwa imefunga mabao 81 na kuwa na safu bora zaidi ya ushambuliaji katika ligi hiyo. Kwa sasa, ushindi katika michezo mitatu ijayo unaweza kuwahakikishia ubingwa na kurejea katika Premier League kwa mara ya kwanza baada ya miaka 25.

Mafanikio hayo hayajapita bila kutambuliwa, ambapo Nicky Butt ameibuka hadharani kumuunga mkono Lampard kurejea Chelsea. Butt anaamini klabu hiyo inapaswa kuwaamini tena mastaa wake wa zamani na kumpa Lampard nafasi ya kuinoa timu hiyo kabla ya kumalizika kwa msimu huu.

Wakati Coventry ikiwa karibu kufikia mafanikio makubwa ya kupanda daraja, na sauti zenye ushawishi zikiongezeka zikimtaka kurejea Stamford Bridge, kurejea kwa makali kwa Lampard kunazidi kuwa moja ya simulizi zinazovutia zaidi katika ulimwengu wa soka kwa sasa.

Lampard balaa jipya mjini.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
2h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
6h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
7h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
9h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
12h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
12h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
12h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
14h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
18h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’