International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumamosi March 28 2026

Joel JJ By Joel JJ
28 Mar 2026
Tetesi za usajili Ulaya, Jumamosi March 28 2026

Soko la usajili barani Ulaya linaendelea kupamba moto huku vilabu vikubwa vikisaka vipaji vipya au kuimarisha vikosi vyao kabla ya dirisha la majira ya joto. Hizi hapa ni tetesi kuu zinazotikisa vichwa vya habari leo:


Arsenal, City, United na Chelsea wamvizia Elliot Anderson

Kiungo wa Nottingham Forest, Elliot Anderson (23), ameibuka kuwa mmoja wa wachezaji wanaowindwa zaidi kwa sasa. Arsenal wanaongoza mbio za kumtaka, lakini wanakabiliwa na ushindani mkali kutoka Manchester City, Manchester United na Chelsea.
Chanzo: CaughtOffside


Manchester United wamfuatilia Adam Wharton

Manchester United wanaendelea kufuatilia kwa karibu kiungo wa England Adam Wharton (22), ambaye yuko tayari kuondoka Crystal Palace ili kujiunga na klabu inayoshiriki UEFA Champions League.
Chanzo: The Sun


Brighton wapunguza bei ya Carlos Baleba

Brighton & Hove Albion wameanza kulegeza msimamo wao kuhusu kiungo Carlos Baleba (22). Badala ya pauni milioni 100 walizokuwa wanadai, sasa wako tayari kusikiliza ofa ya chini zaidi.
Chanzo: The Sun


Mbio za Tchouameni zapamba moto

Kiungo wa Real Madrid, Aurélien Tchouaméni (26), anawindwa na Manchester United pamoja na Liverpool.
Chanzo: Fichajes


Arsenal na Liverpool wagonga mwamba kwa Kvaratskhelia

Arsenal na Liverpool wamepata pigo katika harakati zao za kumchukua winga wa Paris Saint-Germain, Khvicha Kvaratskhelia (25).
Chanzo: Teamtalk


Manchester United wapewa nafasi ya kumsajili Ferran Torres

Manchester United wamepewa nafasi ya kumsajili mshambuliaji wa Hispania Ferran Torres (26) kutoka Barcelona msimu huu wa joto.
Chanzo: Teamtalk


Juventus wamuwania Lewandowski na Greenwood

Juventus wanataka kumsajili mshambuliaji mkongwe Robert Lewandowski (37) kwa uhamisho wa bure endapo ataondoka Barcelona.

Pia wanamfuatilia Mason Greenwood (24), lakini Atlético Madrid nao wanapambana kumsajili kutoka Olympique de Marseille.
Chanzo: La Gazzetta dello Sport


Luis Enrique aipa mgongo Manchester United

Kocha wa Paris Saint-Germain, Luis Enrique (55), anatarajiwa kukataa ofa ya Manchester United na badala yake kusaini mkataba mpya kuendelea PSG.
Chanzo: i Paper


Tottenham wafikiria Sean Dyche

Tottenham Hotspur wanaweza kumgeukia Sean Dyche (54) kusaidia timu kujinasua na hatari ya kushuka daraja, iwapo Roberto De Zerbi (46) ataendelea kushikilia msimamo wake wa kujiunga nao baadaye.
Chanzo: Telegraph


Everton wamtengea mkataba mpya Moyes

Kutokana na mafanikio ya kuibadilisha timu, Everton wanapanga kumpa kocha David Moyes (62) mkataba mpya baada ya kuibadilisha timu kutoka hatari ya kushuka daraja hadi ushindani wa nafasi za Ulaya.
Chanzo: Guardian

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
2h ago
READ MORE →
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
2h ago
READ MORE →
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
3h ago
READ MORE →
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
4h ago
READ MORE →
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
4h ago
READ MORE →
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
5h ago
READ MORE →
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE →
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE →
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE →
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
20h ago
READ MORE →