Simba yamkomalia Damaro, shauri la uraia lasogezwa mbele TFF

Joel JJ By Joel JJ • 28th March 2026


Simba yamkomalia Damaro, shauri la uraia lasogezwa mbele TFF

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limeahirisha hadi wiki ijayo shauri lililofunguliwa na Simba SC dhidi ya mchezaji wa Yanga Mohamed Damaro Camara kuhusiana na uraia wa kiungo huyo.

Imeelezwa sababu ya kuahirishwa ni kuchelewa kwa Yanga na mchezaji Damaro kupokea wito rasmi wa kuhudhuria kikao cha Kamati ya Hadhi na Sheria za Wachezaji za TFF.

Simba imefungua shauri hili ikidai kuwa Yanga wamekiuka kanuni za ligi kwa kuwa na wachezaji 13 wa kigeni, huku kanuni zikiruhusu wachezaji 12 tu.

Mohamed Damaro Camara anacheza kama mchezaji wa Tanzania, jambo ambalo Simba wanasema ni kinyume na taratibu za FIFA kuhusu kubadili uraia wa mchezaji (switching of nationality).

Kwa mujibu wa Simba, hatua hiyo ya Damaro kucheza kama Mtanzania bila kufuata mchakato rasmi wa FIFA inakiuka kanuni za mashindano.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.