Local,Normal News,Azam, Simba

Azam Fc yaipeleka dabi ya Mzizima Azam Complex

Joel JJ By Joel JJ
β€’
28 Mar 2026
Azam Fc yaipeleka dabi ya Mzizima Azam Complex

Mchezo wa ligi kuu ya NBC kati ya Azam Fc dhidi ya Simba maarufu Mzizima Derby ambao umepangwa kupigwa Jumapili ya Apri 05, 2026, utapigwa katika uwanja wa Azam Complex, Chamazi.

Azam Fc ambao ndio wenyeji wa mchezo huo, wamechagua kutumia uwanja wao wa nyumbani, Azam Complex na sio uwanja wa Benjamin Mkapa kama ilivyozoeleka.

Awali kulikuwa na tetesi kuwa mchezo huo ungepigwa 'Lupaso' kama ilivyozoeleka lakini licha ya Serikali kuridhia matumizi ya dimba la Mkapa kwenye baadhi ya mechi, wauza Ice Cream hao wamechagua kupeleka mechi Chamazi dhamira yao ikiwa kuzisaka alama tatu zaidi kuliko mapato.

Mechi ya duru ya kwanza iliyopigwa Disemba 07 2025 Simba wakiwa wenyeji, ilipigwa uwanja wa Benjamin Mkapa na Azam Fc kuibuka na ushindi wa mabao 2-0.

Wakati huu timu hizo zinakutana tena kila moja ikihitaji alama tatu ili kujiweka kwenye nafasi nzuri kwenye mbio za ligi kuu.

Azam FC na Simba zinatofautiana alama mbili tu kwenye msimamo wa ligi, Simba ikiwa nafasi ya pili na alama 31 wakati Azam Fc wako nafasi ya tatu wakiwa na alama 29.

Hata hivyo Azam Fc wamecheza mechi moja zaidi ya Simba hivyo kuwa na uhitaji wa kushinda mchezo huo ili kupunguza gap la pointi dhidi ya wapinzani wao hao.

Azam Fc inayonolewa na kocha Florent Ibenge, msimu huu imeimarika zaidi ikimaliza mechi 15 za duru ya kwanza bila ya kupoteza.

Ni Azam Fc na Yanga pekee ambazo hazijapoteza mchezo wa ligi kuu msimu huu. Hata hivyo wanakwenda kukutana na Simba iliyoimarika zaidi baada ya maboresho waliyofanya kwenye usajili wa dirisha dogo.

Ujio wa kocha Steve Barker na usajili wa wachezaji kama Ismael Toure, Libasse Gueye, Anicet Oura, Inno Loemba na Clatous Chama umeiongezea Simba makali.

Baada ya kulikosa taji la ligi kuu kwa misimu minne mfululizo, Wekundu hao wa Msimbazi msimu huu wamepania kushinda taji hilo ambalo kwa muda wote huo limeishi kwenye makabati ya watani zao wa jadi, klabu ya Yanga.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
14m ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
3h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
5h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
7h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
9h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
10h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
10h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
12h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
15h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
23h ago
READ MORE β†’