International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumapili March 29 2026

Joel JJ By Joel JJ
β€’
29 Mar 2026
Tetesi za usajili Ulaya, Jumapili March 29 2026

Dirisha la usajili linazidi kupamba moto huku vilabu vikubwa vya Ulaya vikianza kupanga mikakati ya kuimarisha vikosi vyao. Hizi hapa ni tetesi kuu za leo kutoka vyombo mbalimbali vya habari:


Newcastle wamuwinda James Trafford

Newcastle United wanaendelea kuonyesha nia ya kumsajili mlinda lango wa England James Trafford (23), iwapo ataamua kuondoka Manchester City.
Chanzo: Football Insider


Sean Dycheakanusha kujiunga Tottenham

Kocha Sean Dyche amekanusha taarifa zinazomuhusisha na kuchukua nafasi ya Igor Tudor katika Tottenham Hotspur.
Chanzo: Talksport


Evan Ndicka awindwa na vigogo Ulaya

Beki wa AS Roma, Evan Ndicka (26), yuko kwenye rada za Barcelona, Tottenham Hotspur, Liverpool na Manchester United. Roma wako tayari kuuza kwa dau linalozidi pauni milioni 39.
Chanzo: CaughtOffside


Nyakossi avutia vilabu vya England

Beki wa Uswisi Roggerio Nyakossi (22), anayekipiga OH Leuven, anawindwa na Liverpool na Chelsea huku mkataba wake ukielekea ukingoni.
Chanzo: The Sun


Marcos Llorente ataka kubaki Atletico

Kiungo Marcos Llorente (31) anatarajiwa kuendelea kubaki AtlΓ©tico Madrid, akiwa kwenye mazungumzo ya kusaini mkataba mpya licha ya kuvutiwa na vilabu vya Premier League.
Chanzo: Fichajes


Real Madrid wamfuatilia Adam Wharton

Real Madrid ni miongoni mwa vilabu vinavyomfuatilia kiungo wa Crystal Palace, Adam Wharton (22), ambaye thamani yake inaendelea kupanda kwa kasi.
Chanzo: AS


Schlotterbeck karibu kuongeza mkataba Dortmund

Beki wa Ujerumani Nico Schlotterbeck (26), ambaye alikuwa akiwindwa na Liverpool na Real Madrid, anakaribia kusaini mkataba mpya na Borussia Dortmund utakaomuweka klabuni hadi mwaka 2031.
Chanzo: Florian Plettenberg

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
3h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
3h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
4h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
4h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
5h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
6h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
6h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
20h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
21h ago
READ MORE β†’