Local,Normal News,Yanga, Prisons

Yanga kuingia kambini leo kuiwinda Tanzania Prisons

Joel JJ By Joel JJ
β€’
30 Mar 2026
Yanga kuingia kambini leo kuiwinda Tanzania Prisons

Meneja wa habari na Mawasiliano wa Yanga Ali Kamwe amesema kikosi cha Yanga leo Jumatatu kinaingia kambini kuanza maandalizi ya mchezo wa ligi kuu dhidi ya Tanzania Prisons ambao utapigwa Jumamosi, April 04 katika uwanja wa KMC Complex.

Kamwe amesema Yanga inarejea mazoezini ikiwa na nyota wote ambao hawakuhusika na majukumu ya timu za Taifa katika kalenda ya FIFA.

"Timu inaingia kambini Jumatatu (leo) kuanza maandalizi ya mchezo wetu unaofuata kwa mujibu wa ratiba ambao ni dhidi ya Tanzania Prisons."

"Mchezo huo utapigwa uwanja wa KMC Comples siku ya Jumamosi, April 04 saa 12:30 jioni."

"Baada ya mapumziko tunatarajia wachezaji wetu wote ambao hawakuwa na majukumu ya timu za Taifa na wale ambao hawana changamoto za majeruhi, wataingia kambini na ari kubwa kujiandaa na mchezo huo," alisema Kamwe.

Akizungumzia taarifa ya wachezaji majeruhi, Kamwe amesema mshambuliaji Prince Dube, beki Ibrahim Bacca, Chadrack Boka na Edmund John wanatarajiwa kuungana na wenzao kwenye mazoezi wakianza na mazoezi ya Gym.

Kamwe amesema mshambuliaji Laurindo Aurelio 'Depu' bado anaendelea kuwa chini ya uangalizi wa daktari na pengine anaweza kuanza mazoezi baada ya wiki moja.

Aidha Kamwe amethibitisha wachezaji Dickson Job na Clement Mzize wameondolewa kwenye mipango ya timu kwa mechi zilizobaki msimu huu kutokana na hali zao baada ya kufanyiwa upasuaji Afrika Kusini.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
45m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’