Meneja wa habari na Mawasiliano wa Yanga Ali Kamwe amesema kikosi cha Yanga leo Jumatatu kinaingia kambini kuanza maandalizi ya mchezo wa ligi kuu dhidi ya Tanzania Prisons ambao utapigwa Jumamosi, April 04 katika uwanja wa KMC Complex.
Kamwe amesema Yanga inarejea mazoezini ikiwa na nyota wote ambao hawakuhusika na majukumu ya timu za Taifa katika kalenda ya FIFA.





