Katika pambano muhimu linaloendelea kuvutia umakini mkubwa wa mashabiki wa soka duniani, timu ya taifa ya Democratic Republic of the Congo imeingia hatua ya mwisho ya intercontinental playoff itakayowapa nafasi ya kufuzu kwa FIFA World Cup kwa mara ya kwanza tangu 1974.
Ushindi dhidi ya Jamaica usiku wa leo utaiwezesha Congo kuendelea moja kwa moja hadi fainali za Kombe la Dunia nchini Marekani, Mexico na Canada.
Pambano la mwisho la kufuzu litachezwa leo Jumanne, Machi 31, 2026 katika Estadio Akron, Guadalajara, Mexico, kuanzia saa 6 usiku kwa saa za Afrika Mashariki. Congo DR wataumana na Jamaica kuwania tiketi moja tu ya kufuzu fainali za Kombe la Dunia 2026.
DR Congo walipata nafasi hii ya intercontinental playoff baada ya kuiondoa Nigeria katika hatua ya CAF playoff ya Afrika. Jamaica hawaendi mchezo huu kama washindi wa moja kwa moja, bali baada ya kuibuka na ushindi wa 1β0 juu ya New Caledonia, na hivyo kuhakikisha nafasi yao kwenye fainali ya intercontinental playoff.
Kwa Congo DR, hii ni safari ya kisoka yenye uzito wa kihistoria. Taifa hilo limepoteza nafasi ya kufuzu kwa Kombe la Dunia kwa zaidi ya miongo 50, tangu walipojulikana kama Zaire na kushiriki mwaka 1974. Kushinda mchezo huu kutakuwa ni mafanikio makubwa si tu kwa soka ya Congo, bali kwa Afrika kwa ujumla.
Kwa upande wa Jamaica, mshindi wa CONCACAF atajitahidi kuikosesha Congo nafasi hiyo, wakijulikana kama timu yenye uwezo wa kucheza compact, haswa kutokana na namna walivyoshinda mchezo wao dhidi ya New Caledonia uliowapa tiketi.