Beki wa Chelsea FC, Marc Cucurella, ametoa maoni mazito kuhusu maamuzi ya hivi karibuni ya klabu, akieleza kuwa baadhi ya hatua zimeathiri morali ya wachezaji.
Cucurella amekiri kuwa kuondoka kwa kocha Enzo Maresca kulikuwa na athari kubwa ndani ya kikosi, akisisitiza kuwa asingependelea uamuzi huo kufanyika katikati ya msimu.
“Kuondoka kwa Maresca kulikuwa na athari kubwa kwetu. Haya ni maamuzi ya klabu, lakini kama ungeuliza mimi, nisingefanya hivyo. Kwa mabadiliko kama hayo, ni bora kusubiri hadi mwisho wa msimu,” alisema.
Aidha, alizungumzia sera ya klabu ya kusajili wachezaji chipukizi, akisema anaelewa mwelekeo huo lakini unaweza kuwa changamoto kwa timu inayolenga kushinda mataji makubwa.
“Ninaelewa hii ni sehemu ya sera ya klabu, kusajili vijana na kuangalia mustakabali. Lakini kwa sisi tuliosalia na tunataka kushinda makombe makubwa, nyakati kama hizi zinakatisha tamaa,” aliongeza.
Cucurella alisisitiza kuwa licha ya Chelsea kuwa na msingi mzuri wa kikosi, bado kuna haja ya kuongeza uzoefu ili kuweza kushindana kwa mafanikio katika Premier League na UEFA Champions League.
“Tunayo msingi mzuri wa wachezaji, lakini kupigania mataji makubwa unahitaji zaidi. Kusajili vijana pekee kunaweza kufanya iwe vigumu kufikia malengo hayo,” alihitimisha.
(Taarifa: @TheAthleticFC)



