Local,Normal News,Yanga

Depu ashusha presha Yanga

Joel JJ By Joel JJ
β€’
31 Mar 2026
Depu ashusha presha Yanga

Mashabiki wa Yanga SC wanapumua kwa faraja baada ya Laurindo Aurelio 'Depu', mshambuliaji hatari kutoka Angola, kuanza mazoezi na kikosi chake.

Hii habari njema kwa Wananchi kwani wanarejesha nguvu zao kuelekea mizunguko ya ligi inayofuata na mapambano ya kutetea ubingwa.

Depu alikuwa nje ya uwanja akiuguza majeraha ya misuli, jambo lililosababisha hofu kidogo miongoni mwa mashabiki kwamba angekaa nje kwa muda mrefu.

Lakini kwa kuonyesha uthabiti na juhudi, mshambuliaji huyu amepambana kuhakikisha anarejea mapema, akiwa tayari kupambana kwenye mechi zijazo.

Akiwa amesajiliwa Yanga katika dirisha dogo la usajili, Depu anaonekana kuwa kinara wa mabao. Katika mechi 10 za mashindano mbalimbali, amefunga mabao 11, ikiwa ni takwimu ya kutisha kwa wapinzani. Kwenye ligi ya NBC, yuko sawa na mshambuliaji mwenzake Prince Dube, kila mmoja akiwa na mabao 6.

Pia ni furaha kubwa kwa Yanga kwamba wachezaji wengine waliokuwa majeruhi tayari wamerejea kikosini, wakiwemo beki tegemeo Ibrahim Hamad Bacca, pamoja na Chadrack Boka na Edmun John.Β 

Kikosi cha Yanga kilirejea mazoezini jana kujiandaa na mchezo wa ligi kuu dhidi ya Tanzania Prisons ambao utapigwa Jumamosi, April 04 uwanja wa KMC Complex.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
46m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’