Simba yajifua kuiwinda Coastal Union

Joel JJ By Joel JJ β€’ 31st March 2026


Simba yajifua kuiwinda Coastal Union

Kikosi cha Simba kinajifua Mo Simba Arena kujiandaa na mchezo wa ligi kuu dhidi ya Coastal Union ambao utapigwa Alhamisi, April 02 katika uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo.

Huu ni moja ya mechi mbili za viporo ambazo Simba itacheza ili kukamilisha mechi za mzunguuko wa kwanza.

Mchezo mwingine wa mzunguuko wa kwanza ambao bado haujapangiwa tarehe ni dhidi ya TRA United ambao awali ulishindwa kufanyika uwanja wa Sheikh Amri Abeid baada ya uwanja huo kujaa maji.

Simba ilirejea mazoezini siku ya Ijumaa kwa ajili ya maandalizi ya mchezo huo ambao Mnyama anazihitaji alama zote tatu ili kupunguza zaidi gap la pointi dhidi ya watani zao Yanga.

Simba iko nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi ikiwa na alama 31 alama saba nyuma ya Yanga yenye alama 38. Lakini kama Simba itashinda mechi hizi mbili za viporo maana yake gap la pointi litabaki alama 1 tu.

Coastal Union ni miongoni mwa timu zisizotabirika kila zinapokutana na Simba. Msimu uliopita walichukua alama moja kwa Simba dimba la KMC Complex kabla ya kufumuliwa mabao 3-0 kwenye mchezo wa duru ya pili uliopigwa Tanga uwanja wa Mkwakwani.

Simba inayonolewa na kocha Steve Barker imekuwa na mwendelezo mzuri kwenye uwanja wa nyumbani, mchezo uliopita wakiifumua TRA United mabao 3-0.

Chini ya Barker ambaye alijiunga na Simba mwishoni mwa Disemba 2025, Wekundu hao wa Msimbazi wametoka sare mechi moja tu kwenye uwanja wa nyumani ikiwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Mtibwa Sugar.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.