Local,Normal News,Azam, Singida

Makocha Singida BS, Azam Fc watambiana

Joel JJ By Joel JJ
β€’
31 Mar 2026
Makocha Singida BS, Azam Fc watambiana

Kocha Mkuu wa Singida Black Stars, Othmen Najjar, amesema kikosi chake kimekamilisha maandalizi kwa umakini mkubwa kuelekea mchezo wao wa ligi kuu dhidi ya Azam FC utakaopigwa kesho Jumatano April 1 katika uwanja wa Airtel huko Singida.

Najjar ameeleza kuwa wamejikita zaidi katika kuimarisha mbinu za ushambuliaji na ulinzi, huku akiwataka wachezaji wake kucheza kwa nidhamu, umakini na kujiamini ili kupata matokeo chanya.

Kwa upande wake, winga wa Singida Black Stars, Ayoub Lyanga, amesema lengo lao kubwa ni kuhakikisha wanaitumia vyema faida ya kucheza nyumbani kwa kupata ushindi.

Nae mkufunzi wa Azam Fc Florent Ibange amesema wanajua wanakwenda kukabiliwa na mechi ngumu mbele ya Singida BS watakaokuwa kwenye uwanja wa nyumbani.

Hata hivyo Ibenge amesema amekiandaa kikosi chake kikamilifu kuweza kuibuka na ushindi.

"Haitakuwa mechi nyepesi, Singida BS sio timu ndogo, msimu uliopita sisi (Azam Fc) tulimaliza nafasi ya tatu na Singida ya nne. Sote tumecheza kombe la Shirikisho (CAFCC) na kufika hatua ya makundi. Hivyo kesho itakuwa mechi kubwa inayozikutanisha timu ambazo ziliiwakilisha Tanzania kwenye mashindano ya CAF"

"Najua hatujawa na mfululizo wa matokeo mazuri mbele ya Singida BS hapa lakini niseme tumekuja kubadili historia hiyo, tuko hapa kwa ajili ya kushinda," alisema Ibenge

Beki wa Azam Fc, Nathaniel Chilambo amesema kwa maandalizi waliyonayo hawahitaji kupoteza mchezo huo wala kupata sare na badala yake ni kupata ushindi.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
5h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
9h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
11h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
13h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
15h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
15h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
16h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
18h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
21h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’