Kiungo mshambuliaji wa Yanga, Pacome Zouzoua, amewapa matumaini mashabiki wa timu hiyo kufuatia matokeo yasiyoridhisha ya hivi karibuni kwenye Ligi Kuu ya Tanzania Bara.
Pacome ameweka wazi kuwa wachezaji wa timu hiyo wanatambua deni kubwa walilonalo kwa mashabiki wao, na wamejipanga kuhakikisha wanarejea kwenye ubora wao haraka iwezekanavyo.





