Pacome Zouzoua Atoa Ujumbe wa Kishujaa kwa Mashabiki wa Yanga

Joel JJ By Joel JJ • 1st April 2026


Pacome Zouzoua Atoa Ujumbe wa Kishujaa kwa Mashabiki wa Yanga

Kiungo mshambuliaji wa Yanga, Pacome Zouzoua, amewapa matumaini mashabiki wa timu hiyo kufuatia matokeo yasiyoridhisha ya hivi karibuni kwenye Ligi Kuu ya Tanzania Bara.

Pacome ameweka wazi kuwa wachezaji wa timu hiyo wanatambua deni kubwa walilonalo kwa mashabiki wao, na wamejipanga kuhakikisha wanarejea kwenye ubora wao haraka iwezekanavyo.

Akizungumza kwa kujiamini, Pacome alikiri kuwa msimu huu umekuwa na changamoto, lakini akaweka bayana kuwa bado kuna nafasi ya kurekebisha mambo:

"Msimu huu umekuwa mgumu kidogo lakini bado haujaisha. Haya ni mambo ya kawaida kwenye mpira na hata kwenye maisha ya kawaida ziko nyakati za kupita vipindi vigumu."

Nyota huyo alieleza kuwa kikosi kizima cha Yanga kimeanza mazoezi kwa ari mpya, kikilenga kurejesha kiwango chao bora:

"Jambo muhimu ni kukubali hali hii na kuongeza bidii uwanja wa mazoezi ili kuhakikisha tunarejea tukiwa imara zaidi."

"Tumerejea mazoezini tukiwa na umakini mkubwa, tutafanya mazoezi kwa bidii ili turejee kwenye ubora wetu na kuwapa furaha mashabiki," alisema

Yanga sasa wanajiandaa kwa mchezo wa ligi dhidi ya Tanzania Prisons utakaopigwa katika dimba la KMC Complex siku ya Jumamosi.

Mchezo huo utakuwa kipimo kwa mabingwa hao watetezi kuona kama wako tayari kutetea ubingwa kwa msimu wa tano mfululizo baada ya sare tatu mfululizo kabla ya mapumziko ya kalenda ya FIFA.

Katika mpango wa kuboresha zaidi, Yanga ilimrejesha aliyekuwa Mkurugenzi wa ufundi Abdulhamid Moalin wakimkaidhi majukumu ya kocha msaidizi ili kumsaidia Pedro Goncalves alikiri kuwa na wakati mgumu hasa kwenye mechi za ugenini.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.