International,Normal News,Local, Ghana, FIFA

Regragui Ahusishwa na Kuinoa Ghana

Joel JJ By Joel JJ
β€’
1 Apr 2026
Regragui Ahusishwa na Kuinoa Ghana

Chama cha Soka cha Ghana (GFA) kimeanza mazungumzo na kocha wa zamani wa Morocco Walid Regragui, kuhusu uwezekano wa kuinoa timu ya taifa ya nchi hiyo, maarufu kama Black Stars.

Taarifa kutoka vyombo mbalimbali vya habari barani Afrika zinaeleza kuwa Regragui ni miongoni mwa makocha wanaopewa nafasi kubwa ya kushika wadhifa huo, huku mazungumzo kati yake na GFA yakiwa tayari yameanza, ingawa bado hakuna makubaliano rasmi yaliyofikiwa.

Hatua hiyo ya GFA inakuja kufuatia mabadiliko ya benchi la ufundi baada ya kuondoka kwa aliyekuwa kocha wa timu hiyo, Otto Addo hali iliyochangiwa na matokeo yasiyoridhisha katika mechi za hivi karibuni za kimataifa.

Walid Regragui anatajwa kuwa chaguo bora kutokana na rekodi yake nzuri, hasa baada ya kuiongoza Morocco kufika hatua ya nusu fainali ya Kombe la Dunia 2022, mafanikio yaliyoweka historia kwa bara la Afrika.

Hata hivyo, kocha huyo aliondoka hivi karibuni kuinoa Morocco kufuatia changamoto zilizojitokeza baada ya mashindano ya Africa Cup of Nations 2025.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, ushindani wa nafasi hiyo ni mkubwa huku makocha wengi kutoka ndani na nje ya Afrika wakitajwa kuwania kibarua hicho.

Endapo Walid Regragui atateuliwa, anatarajiwa kupewa jukumu la kuiandaa GhanaΒ kwa mashindano yajayo ya kimataifa ikiwemo FIFA World Cup 2026.

Hadi sasa, GFA haijatoa tamko rasmi kuhusu uteuzi wa kocha mpya.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
46m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’