Local,Normal News,Simba, Yanga

TFF yatupilia mbali shauri la Simba dhidi ya Damaro

Joel JJ By Joel JJ
β€’
2 Apr 2026
TFF yatupilia mbali shauri la Simba dhidi ya Damaro

Sakata la usajili wa kiungo wa Yanga, Mohamed Damaro Camara, limechukua sura mpya baada ya Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kulitupilia mbali rasmi shauri lililowasilishwa na klabu ya Simba SC.

Kupitia taarifa iliyotolewa Aprili 2, 2026 na Ofisa Habari na Mawasiliano wa TFF, Cliford Mario Ndimbo, kamati hiyo imebainisha kuwa haina sababu za kuendelea na shauri hilo baada ya kubaini kuwa usajili wa mchezaji huyo uko halali na haukiuki kanuni zilizotajwa.

Simba walikuwa wamefungua malalamiko wakidai kuwa usajili wa Damaro unaifanya Yanga kuwa na idadi ya wachezaji wa kigeni 13, kinyume na kanuni zinazoruhusu wachezaji 12 pekee kwa kila timu ya Ligi Kuu.

Aidha, klabu hiyo ilieleza kuwa usajili huo unakiuka Kanuni ya 62(1) ya Ligi Kuu pamoja na taratibu za usajili zilizoainishwa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA).

Katika uamuzi wake, Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji imeeleza wazi kuwa hoja zilizowasilishwa na Simba hazina msingi wa kisheria kwa mujibu wa kanuni husika, na kwamba mchezaji huyo habanwi na masharti yaliyotajwa katika malalamiko hayo.

Hivyo, kwa mujibu wa kamati hiyo, usajili wa Mohamed Damaro Camara uko sahihi na unakidhi vigezo vyote vya kikanuni.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
43m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’