Kiungo mshambuliaji wa Simba Elie Mpanzu anatarajiwa kukosa mchezo wa ligi kuu dhidi ya Coastal Union ambao utapigwa leo Alhamisi, April 02 katika uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo jijini Dar es salaam.
Taarifa kutoka ndani ya uongozi wa Simba imebainisha kuwa Mpanzu nakosekana kwenye mchezo huo kutokana na changamoto ya kuugua.
Mkufunzi wa Simba Steve Barker amempa mapumziko Mcongomani huyo ili aweze kuimarika zaidi.
Hata hivyo Mpanzu anaweza kurejea kikosini kwenye maandalizi ya Derby ya Mzizima ambapo Simba itaumana na Azam Fc uwanja wa Azam Complex siku ya Jumatano



