Mpanzu akwama kuivaa Coastal Union, sababu yatajwa

Joel JJ By Joel JJ β€’ 2nd April 2026


Mpanzu akwama kuivaa Coastal Union, sababu yatajwa

Kiungo mshambuliaji wa Simba Elie Mpanzu anatarajiwa kukosa mchezo wa ligi kuu dhidi ya Coastal Union ambao utapigwa leo Alhamisi, April 02 katika uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo jijini Dar es salaam.

Taarifa kutoka ndani ya uongozi wa Simba imebainisha kuwa Mpanzu nakosekana kwenye mchezo huo kutokana na changamoto ya kuugua.

Mkufunzi wa Simba Steve Barker amempa mapumziko Mcongomani huyo ili aweze kuimarika zaidi.

Hata hivyo Mpanzu anaweza kurejea kikosini kwenye maandalizi ya Derby ya Mzizima ambapo Simba itaumana na Azam Fc uwanja wa Azam Complex siku ya Jumatano


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.