Ili tushinde ni lazima tuwe bora kuliko Simba - Ibenge

Joel JJ By Joel JJ β€’ 4th April 2026


Ili tushinde ni lazima tuwe bora kuliko Simba - Ibenge

Kocha Mkuu wa Azam Fc Florent Ibenge amesema mechi ya ligi kuu dhidi ya Simba itakayopigwa kesho Jumapili katika uwanja wa Azam Complex, inazikutanisha timu bora ambazo ziliiwakilisha Tanzania katika michuano ya CAF msimu huu.

Ibenge amesema ili kuweza kushinda mchezo huo watalazimika kupandisha kiwango chao na kuwazidi Simba.

"Simba Sc sio timu ndogo, ni miongoni mwa timu bora kabisa hapa Tanzania, ukiangalia vile wanavyocheza ni wazi utaona wanacheza vizuri"

"Ni timu nzuri, hivyo mechi dhidi ya Simba sio sawa na mechi unazocheza dhidi ya timu nyingine"

"Walikuwa hatua ya makundi ligi ya mabingwa (CAFCL) sisi tulikuwa kombe la Shirikisho (CAFCC) hivyo tunakwenda kucheza mechi kubwa itakayokutanisha timu zilizocheza makundi CAF"

"Kucheza mechi za aina hii ni lazima tupandishe kiwango chetu hivyo tutapaswa kuwa bora dhidi ya Simba ili tuweze kuibuka na ushindi," alisema Ibenge


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.