Tetesi za usajili Ulaya, Jumapili April 05 2026

Joel JJ By Joel JJ β€’ 5th April 2026


Tetesi za usajili Ulaya, Jumapili April 05 2026

Tetesi za usajili barani Ulaya zinazidi kushika kasi. Vilabu vikubwa vinaendelea kupimana nguvu katika kuwinda vipaji bora kabla ya dirisha la majira ya joto kufunguliwa rasmi. Hizi hapa ni habari kuu za leo:


Inter Milan Wamvizia Vicario

Inter Milan wanamtaka kipa wa Tottenham Hotspur, Guglielmo Vicario, kuwa chaguo lao kuu langoni msimu ujao (Calciomercato).


Chelsea Wamfuatilia Valentin Barco

Chelsea wana nia ya kumsajili beki chipukizi Valentin Barco kutoka Strasbourg (talkSPORT).


Liverpool Wamtaka Marco Palestra

Liverpool wanapanga kuongeza nguvu upande wa ulinzi kwa kumchukua Marco Palestra wa Atalanta (CaughtOffside).


Manchester United Wamchunguza Atcheson

Manchester United ni miongoni mwa vilabu vinavyomfuatilia beki kijana Tom Atcheson wa Blackburn Rovers (TeamTalk).


Sunderland Wamnyatia Sergio Arribas

Sunderland wanaweza kumsajili kiungo Sergio Arribas kutoka Almeria iwapo mipango yao itatekelezwa (Sport Witness).


Arsenal vs Liverpool kwa Anthony Gordon

Arsenal wanajiandaa kupambana na Liverpool katika kinyang'anyiro cha kumsajili Anthony Gordon wa Newcastle United (Football Transfers).



  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.