Tetesi za usajili barani Ulaya zinazidi kushika kasi. Vilabu vikubwa vinaendelea kupimana nguvu katika kuwinda vipaji bora kabla ya dirisha la majira ya joto kufunguliwa rasmi. Hizi hapa ni habari kuu za leo:
Inter Milan Wamvizia Vicario
Inter Milan wanamtaka kipa wa Tottenham Hotspur, Guglielmo Vicario, kuwa chaguo lao kuu langoni msimu ujao (Calciomercato).
Chelsea Wamfuatilia Valentin Barco
Chelsea wana nia ya kumsajili beki chipukizi Valentin Barco kutoka Strasbourg (talkSPORT).
Liverpool Wamtaka Marco Palestra
Liverpool wanapanga kuongeza nguvu upande wa ulinzi kwa kumchukua Marco Palestra wa Atalanta (CaughtOffside).
Manchester United Wamchunguza Atcheson
Manchester United ni miongoni mwa vilabu vinavyomfuatilia beki kijana Tom Atcheson wa Blackburn Rovers (TeamTalk).
Sunderland Wamnyatia Sergio Arribas
Sunderland wanaweza kumsajili kiungo Sergio Arribas kutoka Almeria iwapo mipango yao itatekelezwa (Sport Witness).
Arsenal vs Liverpool kwa Anthony Gordon
Arsenal wanajiandaa kupambana na Liverpool katika kinyang'anyiro cha kumsajili Anthony Gordon wa Newcastle United (Football Transfers).



