Singida BS yavunja benchi la ufundi baada ya kipigo dhidi ya TRA United

Joel JJ By Joel JJ β€’ 5th April 2026


Singida BS yavunja benchi la ufundi baada ya kipigo dhidi ya TRA United

Klabu ya Singida BS imetangaza kuvunja benchi la ufundi kufuatia mfululizo wa matokeo mabaya.

Taarifa iliyotolewa na timu hiyo siku ya Jumapili, imebainisha kuwa hatua hiyo imechukuliwa mara moja huku wakitarajiwa kutangaza benchi la ufundi la muda.

Singida BS imelifuta benchi la ufundi muda mfupi baada ya kipigo cha mabao 2-0 dhidi ya TRA United katika mchezo uliopigwa uwanja wa Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.