Klabu ya Singida BS imetangaza kuvunja benchi la ufundi kufuatia mfululizo wa matokeo mabaya.
Taarifa iliyotolewa na timu hiyo siku ya Jumapili, imebainisha kuwa hatua hiyo imechukuliwa mara moja huku wakitarajiwa kutangaza benchi la ufundi la muda.
Singida BS imelifuta benchi la ufundi muda mfupi baada ya kipigo cha mabao 2-0 dhidi ya TRA United katika mchezo uliopigwa uwanja wa Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha.




