Timu za Azam FC na Simba SC zimetoka sare ya bila kufungana katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa Jumapili, Aprili 5, 2026, kwenye Uwanja wa Azam Complex Stadium
Mchezo huo uliokuwa na ushindani mkubwa ulizikutanisha timu hizo mbili zinazowania nafasi za juu kwenye msimamo wa ligi, huku kila upande ukionyesha umakini mkubwa hasa katika safu ya ulinzi.
Walinda lango Aishi Manula wa Azam FC na Djibrill Kassali wa Simba kw nyakati tofauti walilazimika kufanya kazi ya ziada kuokoa hatari langoni. Makipa hao walifanya mfululizo wa uokoaji na kuzuia mashuti ya hatari yaliyolenga nyavu zao.
Katika eneo la kiungo, kulishuhudiwa mapambano makali ya kumiliki mpira ambapo Azam FC walimtegemea James Akaminko, Himid Mao na Feisal Salum, huku Simba SC wakijibu mapigo kupitia Yusuph Kagoma, Allasane Kante pamoja na Clatous Chama.
Katika kipindi cha pili, Simba walifanya mabadiliko kwa kumtoa Chama na nafasi yake kuchukuliwa na Neo Maema, hatua iliyolenga kuongeza nguvu ya ushambuliaji, lakini haikuzaa matunda yaliyotarajiwa.
Licha ya kumalizika kwa sare ya bila mabao, mchezo huo ulikuwa wa wazi na wenye kasi, huku kila timu ikitengeneza nafasi kadhaa za kufunga. Hata hivyo, ukosefu wa umakini katika umaliziaji wa nafasi hizo uliwanyima mashabiki fursa ya kushuhudia mabao.



