Katika ujumbe wa umoja na kukemea ubaguzi, Vinícius Júnior, kiungo mshambuliaji mahiri wa klabu ya Real Madrid na timu ya Taifa ya Brazil, ameonyesha sapoti yake kwa Lamine Yamal, nyota kijana wa FC Barcelona, kufuatia matukio ya kauli za ubaguzi zilizosikika uwanjani hivi karibuni.
Hii imejiri baada ya mchezo wa kirafiki wa kimataifa kati ya Hispania na Misri uliochezwa RCDE Stadium mjini Barcelona, ambapo baadhi ya mashabiki waliibua kauli chafu za kinidhamu zinazohusiana na ubaguzi wa kiislamu.
Tukio hilo limesababisha polisi wa Hispania kuanzisha uchunguzi kuhusu chanzo na athari za kauli hizo zenye asili ya ubaguzi wa kikabila na kidini.
Katika hali iliyozua mjadala mkubwa, Yamal, ambaye ni Muislamu, alichukua nafasi kwenye mtandao wa kijamii kueleza hisia zake kuhusu kauli hizo, akisema zilikuwa “haina heshima na zisizovumilika,” licha ya kutambua kuwa zilikuwa zikielekezwa kwa wapinzani wao wa uwanjani na si yeye binafsi.
Katika ujumbe wake wa kuonyeshamshikamano, Vinícius Jr aliendelea kuonyesha msaada kwa kijana huyo wa Barcelona, akizungumza kuhusu umuhimu wa vita dhidi ya ubaguzi unaoendelea kuibuka katika soka la Ulaya.
Kiungo huyo mshambuliaji, ambaye yeye mwenyewe amekuwa akipigwa vita na kauli chafu za ubaguzi nchini Hispania katika miaka ya hivi karibuni, aliitaka jamii ya wachezaji kuungana dhidi ya vitendo vya ubaguzi na kushirikiana kupambana navyo.



