Local,Normal News,Yanga, Pamba

KOCHA YANGA AIHOFIA PAMBA JIJI

Joel JJ By Joel JJ
7 Apr 2026
KOCHA YANGA AIHOFIA PAMBA JIJI

Kocha Mkuu wa Young Africans SC, Pedro Goncalves, amesema mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Pamba Jiji FC utakaopigwa kesho Jumatano, Aprili 8, katika Uwanja wa CCM Kirumba Stadium utakuwa mgumu kutokana na uimara wa wapinzani wao wanapocheza nyumbani.

Akizungumza na waandishi wa habari kuelekea mchezo huo, Goncalves alisema Pamba Jiji imejijengea rekodi ya kutopoteza mechi yoyote katika uwanja wake, jambo linaloifanya kuwa timu hatari hasa inapocheza mbele ya mashabiki wake.

“Tunakwenda kukutana na timu yenye ushindani mkubwa na imara wanapocheza nyumbani. Hawajapoteza mechi katika uwanja wao na timu nyingi kubwa zimekuja hapa bila kupata ushindi,” alisema.

Kocha huyo aliongeza kuwa wanatarajia mchezo wenye ushindani mkubwa na mazingira magumu, akieleza kuwa hali ya uwanja inaweza isiwe rafiki kwa soka la kuvutia, lakini hilo halitabadilisha malengo yao ya kutafuta ushindi.

“Tunapaswa kuwa imara, makini na kupambana ili kuhakikisha tunapata alama tatu,” alisisitiza.

Aidha, Goncalves alibainisha kuwa Pamba Jiji ni timu inayocheza kwa nguvu, kasi na kutumia vizuri faida ya mashabiki wao wa nyumbani, hali inayowalazimu Yanga kujiandaa kisaikolojia na kimkakati.

Katika hatua nyingine, kocha huyo alizungumzia ushindani wa ligi msimu huu, akisema licha ya timu yake kuwa juu ya msimamo, bado kuna safari ndefu mbele.

“Bado tuna michezo mingi na kila timu inapambana kufikia malengo yake, hivyo tunapaswa kuendelea kuwa makini na kufanya kazi kwa bidii,” alisema.

Aliongeza kuwa ana imani kubwa na wachezaji wake na wanahitaji kuonyesha nidhamu, umoja na ari ya kupambana ili kupata matokeo chanya katika mchezo huo.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
5h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
11h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
17h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE →