International,Normal News,Chelsea

Garnacho awachana mastaa wenzake Chelsea

Xtra 90 Media By Xtra 90 Media
β€’
7 Apr 2026
Garnacho awachana mastaa wenzake Chelsea

Winga wa klabu ya Chelsea, Alejandro Garnacho, ametoa kauli kufuatia mjadala ulioibuka baada ya mahojiano ya hivi karibuni, akilenga moja kwa moja hali ya ndani ya kikosi cha Chelsea.

Garnacho amesema kuwa moja ya mambo makubwa aliyojifunza akiwa Manchester United ni umuhimu wa uwajibikaji wa wachezaji na uzalendo katika timu, akidai kuwa hilo linakosekana kwa kiasi kikubwa ndani ya Chelsea kwa sasa.

Ameongeza kuwa baadhi ya wachezaji wanapaswa kukomaa zaidi na kubeba majukumu yao badala ya kulaumiana au kujificha wanapokumbana na changamoto.

“Tazama, moja ya mambo makubwa niliyoyajifunza Manchester United ni kwamba uwajibikaji wa kweli kwa sasa unakosekana ndani ya dressing room ya Chelsea. Binafsi, ninaamini wachezaji wengi wanapaswa kukomaa na kuchukua majukumu zaidi badala ya kulaumiana au kujificha."

"Klabu inapitia kipindi kigumu, kila mtu anaona hilo, lakini huwezi kukimbia au kununa kila mambo yanapokwenda tofauti na matarajio. Hiyo hali ya kujiona bora inapaswa kukoma, inaidhoofisha timu. Hakuna mchezaji aliye mkubwa kuliko klabu. Si mimi, si mtu mwingine yeyote. Unapaswa kuheshimu nembo, unapaswa kumheshimu kocha, vinginevyo hustahili kuvaa jezi hiyo."

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’