Local,Normal News,Yanga, Pamba, Singida, KMC

Mudathir, Okello waimaliza Pamba Jiji

Joel JJ By Joel JJ
β€’
8 Apr 2026
Mudathir, Okello waimaliza Pamba Jiji

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya NBC, Yanga, wameendelea kuonesha ubora wao baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Pamba Jiji katika mchezo uliopigwa Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza.

Katika mchezo huo, Yanga walidhibiti kwa kiasi kikubwa umiliki wa mpira na kutengeneza nafasi nyingi za kufunga. Kiungo Mudathir Yahya alikuwa nyota wa mchezo baada ya kufunga mabao mawili katika dakika ya 8 na 33, kabla ya Maxi Nzengeli kuongeza bao la tatu dakika ya 67 na kuhitimisha ushindi huo mnono.

Kiungo mshambuliaji Allan Okello alikuwa mwiba mkali kwa walinzi wa Pamba Jiji akitoa pasi za mabao yote matatu yaliyofungwa na Yanga.

Ushindi huo unaifanya Yanga kuendelea kujiimarisha kileleni mwa msimamo wa ligi wakifikisha alama 44 wakikaa kileleni kwa tofauti ya alama 9.

Kwa upande wa Pamba Jiji, walionekana kushindwa kuhimili kasi na ubora wa wapinzani wao, licha ya kucheza nyumbani mbele ya mashabiki wao.

Wakati huohuo, katika mchezo mwingine uliochezwa mapema, Singida Black Stars waliibuka na ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya KMC FC.

Mchezo huo ulikuwa na ushindani mkubwa, huku timu zote zikicheza kwa tahadhari. Singida BS walifanikiwa kupata bao pekee la ushindi lililofungwa la Lamine Jarjou kwenye dakika ya 70 na kuwapa alama tatu muhimu.

Singida BS na KMC ziliingia kwenye mchezo huo zikiwa kwenye presha kubwa ya kuhitaji matokeo zote zikiwa zimetimua makocha wao.

More Stories

Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
4h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
4h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
6h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
7h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
10h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
12h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
13h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’
Kocha Dimitar Pantev ateuliwa kuwa kocha mpya wa Richard Bay.
Kocha Dimitar Pantev ateuliwa kuwa kocha mpya wa Richard Bay.
1d ago
READ MORE β†’