Local,Normal News,Simba, TRA, Mbeya City, Azam

TRA United, Simba, Mbeya City, Azam Fc viwanjani leo

Joel JJ By Joel JJ
β€’
9 Apr 2026
TRA United, Simba, Mbeya City, Azam Fc viwanjani leo

Ligi Kuu ya NBC inaendelea leo ambapo mechi mbili zinapigwa mkoani Arusha na Manyara.

Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha kutakuwa na mchezo wa kukata na shoka wenyeji TRA United wakiikaribisha Simba.

Ni mchezo unaosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka mkoani humo hasa ikizingatiwa mchezo huo awali ulipaswa kupigwa March 14 lakini uliahirishwa baada ya mvua kubwa kunyesha na kupelekea kujaza maji uwanja wa Sheikh Amri Abeid.

Wekundu wa Msimbazi wanazihitaji alama zote tatu ili kupunguza gap dhidi ya watani zao Yanga ambao ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Pamba Jiji jana umewafanya wajiimarishe kileleni kwa tofauti ya alama 9.

TRA United wametamba kuwa hakuna timu itatoka salama uwanja wa Sheikh Amri Abeid baada ya kuifunga Singida BS mabao 2-0 katika mchezo uliopita kwenye uwanja huo.

Ikumbukwe pia hata vinara wa ligi Yanga waliacha alama mbili Arusha baada ya kutoka suluhu ya bila kufungana.

Mchezo mwingine utapigwa kule Manyara kati ya Mbeya City dhidi ya Azam Fc. Huu ni mchezo muhimu kwa kila upande Mbeya City nao wakihitaji alama zote tatu ili kujiweka eneo salama na hatari ya kushuka daraja huku Azam Fc wakitambua kama wanakosa ushindi katika mchezo huo, pengine matumaini ya kuwania ubingwa msimu huu yatazidi kufifia.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
5h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
9h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
10h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
12h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
12h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
16h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
18h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
18h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’