International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Alhamisi, April 09 2026

Joel JJ By Joel JJ
β€’
9 Apr 2026
Tetesi za usajili Ulaya, Alhamisi, April 09 2026

Dirisha la usajili majira ya kiangazi linakaribia huku vilabu vikubwa vikianza kuweka wazi malengo yao. Leo, taarifa zinaonyesha harakati kubwa za kuimarisha vikosi, hasa katika Premier League.


Arsenal Waimarisha Ulinzi

Arsenal wanatafuta kuongeza nguvu safu ya ulinzi kwa kulenga kumsajili Victor Valdepenas wa Real Madrid pamoja na Jacobo Ramon wa Como (CaughtOffside).


Martinelli Ang’ang’ania Kubaki Arsenal

Gabriel Martinelli ameweka wazi nia yake ya kuendelea kusalia Arsenal licha ya tetesi za kuuzwa (Football Insider).


Dortmund Wamtaka Tena Jadon Sancho

Borussia Dortmund wanapanga jaribio la tatu kumsajili Jadon Sancho, ambaye yuko kwa mkopo Aston Villa kutoka Manchester United (Telegraph).


Tottenham Wamnyatia Trafford

Tottenham Hotspur wanamtaka James Trafford wa Manchester City kama sehemu ya mipango yao ya usajili (TeamTalk).


Ada Kubwa kwa Elliot Anderson

Nottingham Forest wanataka kati ya pauni milioni 100 hadi 120 kwa Elliot Anderson, anayewindwa na Manchester United na Manchester City (Florian Plettenberg).


Everton Wajaribu Kumuweka Grealish

Everton hawako tayari kulipa pauni milioni 50 kwa Jack Grealish, lakini wanataka kubaki naye kutoka Manchester City (The Athletic).


City Wamfuatilia Kijana Eichhorn

Manchester City wamejiunga na mbio za kumsajili chipukizi Kennet Eichhorn wa Hertha Berlin (Fabrizio Romano).


Leeds Wamruhusu Mateo Joseph Kuondoka

Leeds United wako tayari kumuuza Mateo Joseph baada ya mkopo wake Mallorca (Football Insider).


Chelsea Wamkingia Kifua Acheampong

Chelsea hawana mpango wa kumuuza Josh Acheampong licha ya kucheza mara chache (Express).


Garnacho Aingia Kwenye Radar ya River Plate

Kocha Eduardo Coudet wa River Plate amewasiliana na Chelsea na Alejandro Garnacho kuhusu uwezekano wa mkopo wa mwaka mmoja (TyC / Football London).

More Stories

Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya
Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya
3h ago
READ MORE β†’
LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
5h ago
READ MORE β†’
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
7h ago
READ MORE β†’
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
7h ago
READ MORE β†’
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
8h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
8h ago
READ MORE β†’
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
9h ago
READ MORE β†’
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
16h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
21h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
21h ago
READ MORE β†’