Klabu ya KMC hivi karibuni ilitangaza kuachana na kocha mkuu Abdallah Mohamed “Bares” pamoja na benchi lote la ufundi kufuatia matokeo duni yanayowakabili msimu huu wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Hatua hii imekuja baada ya timu kushika nafasi za chini kwenye jedwali, jambo lililosababisha uongozi kufanya maamuzi hayo ili kuinusuru klabu hiyo na janga la kushuka daraja.





