Local,Transfer News,KMC

Minziro atajwa KMC

Joel JJ By Joel JJ
9 Apr 2026
Minziro atajwa KMC

Klabu ya KMC hivi karibuni ilitangaza kuachana na kocha mkuu Abdallah Mohamed “Bares” pamoja na benchi lote la ufundi kufuatia matokeo duni yanayowakabili msimu huu wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Hatua hii imekuja baada ya timu kushika nafasi za chini kwenye jedwali, jambo lililosababisha uongozi kufanya maamuzi hayo ili kuinusuru klabu hiyo na janga la kushuka daraja.

Kwa sasa, uongozi wa KMC unatafuta kocha mpya atakayechukua nafasi ya benchi la ufundi na kujaribu kubadilisha mwenendo wa timu.

Miongoni mwa majina yanayotajwa ni Fred Felix Minziro maarufu kama “Majeshi”, kocha mwenye uzoefu mkubwa nchini Tanzania. Minziro anatajwa kuwa miongoni mwa wale wanaoweza kuvaa viatu vilivyowashinda makocha waliotangulia, Marcio Maximo na Mohamed Bares.

Minziro anatambulika miongoni mwa makocha wenye mbinu na uwezo wa kuinua kikosi chenye changamoto kubwa, pia akisifika kwa kuzipandisha daraja timu mbalimbali kutoka madaraja ya chini.

KMC wamekusanya alama nane tu msimu katika mechi 18 ni wazi dalili za kuelekea championship zinaonekana na pengine kazi ya ziada inapaswa kufanyika kuwanusuru na janga la kushuka daraja.

More Stories

Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya
Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya
2h ago
READ MORE →
LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
4h ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
6h ago
READ MORE →
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
6h ago
READ MORE →
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
7h ago
READ MORE →
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
8h ago
READ MORE →
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
8h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
16h ago
READ MORE →
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
20h ago
READ MORE →
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
20h ago
READ MORE →