International,Normal News,Local

Aliou Cisse kuinoa Angola

Joel JJ By Joel JJ
9 Apr 2026
Aliou Cisse kuinoa Angola

Shirikisho la Kandanda la Angola (FAF), limekamilisha mazungumzo na kocha Aliou Cissé kutoka Senegal wakimteua kuwa kocha mpya wa timu yao ya taifa, Palancas Negras.

Cissé, ambaye aliongoza timu ya taifa ya Senegal kufikia mafanikio makubwa ikiwemo kufika fainali ya Kombe la Afrika (AFCON) 2021, tayari amekubali kuinoa Angola.

Taarifa kutoka kwa vyanzo vya karibu na shirikisho la kandanda la Angola zinaonyesha kuwa kocha huyo anatarajiwa kuchukua mikoba ya timu hiyo katika hatua za mashindano ya kimataifa.

Cissé anakuja akiwa na uzoefu mkubwa wa kuiongoza timu za taifa, pamoja na safari yake ya hivi karibuni akiwa kocha wa Libya, ambapo aliondoka kutokana na changamoto za kifedha na mkataba.

Mashabiki wa Palancas Negras na wadau wa soka nchini Angola wanatarajia uteuzi wa Cissé uanze kutekelezwa haraka, wakiamini kwamba kocha huyo mwenye uzoefu wa kimataifa atasaidia kuongeza ushindani wa timu ya taifa ya Angola.

More Stories

Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
4h ago
READ MORE →
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
4h ago
READ MORE →
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
6h ago
READ MORE →
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
7h ago
READ MORE →
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
10h ago
READ MORE →
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
12h ago
READ MORE →
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
13h ago
READ MORE →
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE →
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE →
Kocha Dimitar Pantev ateuliwa kuwa kocha mpya wa Richard Bay.
Kocha Dimitar Pantev ateuliwa kuwa kocha mpya wa Richard Bay.
1d ago
READ MORE →